7K Views

Thumbnail

SONG:NAJUTA

ARTISTS:STAMINA FT RICH MAVOKO

PRODUCER:KEVY

STUDIO:SNAP RECORDS

SONG WRITER:STAMINA&RICH MAVOKO

INTRO

Stamina;iz moro town baby,im back,u know wat kevy,this iz so matured meeeen

Vers 1{stamina}

Shida zinaomba urafiki,umasikini unaleta posa

Ukubwa meli ya kigiriki,nimezamia bila boxer

Bikra ya utoto,imeshavunjwa na balehe

Ukubwa una mingi misoto,na mchanganyo wa starehe

Mara ooooh baba kijacho,eti niandae hela ya nepi

Wife anatoa macho,anangoja shopping ya sketi

Hakimu ana nyundo ya noti,mtuhumiwa nasaka chenchi

Bongo mahakama za joti,me mpoki nabaki benchi

Hata nikimchukia baniani,kiatu chake kina mchango

Mzinzi na nyota ya kijani,ndio uzazi usiokua na mpango

Balehe noma,kama baunsa aliyepigwa na mtoto

Ukubwa mechi ya kisodoma,haiwezi chezeshwa na mpoto

Aaaaah kas na kas,ni kasi isiyokua na kasi

Ila nikiweka kas na kus,ndio kusi pacha wa kasi

Bora wewe jalala,me ukubwa shimo la choo

Ukichanganya na ufukara,ndio mechi isiyokua na droo

Choruss{rich mavoko}

Kama nakufuru,mungu naomba unisamehe

Nakosa uhuru,sikumbuki hata tarehe

Kweli najuta kuzijua hizi starehe eeeeeee eeeeeee eeeeeee eeeeeehh

Ehhhh me najuta kubalehe

Ehhhh sikumbuki hata tarehe

Eeee ujana maji ya moto,zinaniunguza hizi starehe

Vers 2{stamina}

Maisha ngumi ya bitozi,siogopi kutega sura

Pesa sitafuti kwa pozi,bado najinyima kula

Nishachoka kusadiki,tomaso tangu na tangu

Marafiki wanafiki,wanasnitch hadi kwa mke wangu

Majukumu ya familia,nimeyabeba bila ngata

Asili zimezidi mia,desturi zimenikamata

Haya maumivu ya mjeledi,kwenye ngozi ya mlemavu

Ukubwa mechi ya mabaamedi,me mlevi nafungwa kavu

Aaaah maisha jabali,ugomvi wa cheka na Tyson

Sikuhizi ukinunua hata kagari,kitaani unaitwa free mason

Maumivu ya sufuria,jikoni hayana ushuru

Pesa tajiri wa dunia,mwenye hisa yangu ya uhuru

Aiseh sayansi imenikera,ukuaji umenipa msoto

Utu uzima bila hela,utamwamkia hadi mtoto

Napopata mkwanja,na shida zinagonga hodi

Vipi nitanunua kiwanja,huku bado nadaiwa kodi

Choruss{rich mavoko}

Kama nakufuru,mungu naomba unisamehe

Nakosa uhuru,sikumbuki hata tarehe

Kweli najuta kuzijua hizi starehe eeeeeee eeeeeee eeeeeee eeeeeehh

Ehhhh me najuta kubalehe

Ehhhh sikumbuki hata tarehe

Eeee ujana maji ya moto,zinaniunguza hizi starehe

Vers 3{stamina}

Ukubwa msafara wa kenge,me mjusi vipi unichoshe

Penzi kitovu cha uzembe,nakaza nisiitwe ngoswe

Ugangstar bila hela,majibu yake ni uchafu

Maisha ya bongo msosi wa jela,so mfungwa usiulizie ndafu

Nilizoea kashata,bumunda na vibagia

Huku unga,bangi,na bapa,ndio vitu navyovisikia

Chuki na fitina,hadhina za wenye wivu

Wapo wanaonishirikina,ili moto nigeuke jivu

Udogoni nilidekezwa,wazazi walinipa malezi

Pesa imesomea udereva,inaendesha hadi mapenzi

Elimu ya njia za panya,inanikosesha michongo

Madeni yananiandama,kama serikali ya bongo

Maishani ukiwa govinda,wenzako watakuita yaya

Pesa mnyama anayewindwa,na jangiri aliyevuta kaya

Uwazi unanidondosha,bado narushiwa kombora

Condom ndio kinga tosha,sijikingi na bastora

Choruss{rich mavoko}

Kama nakufuru,mungu naomba unisamehe

Nakosa uhuru,sikumbuki hata tarehe

Kweli najuta kuzijua hizi starehe eeeeeee eeeeeee eeeeeee eeeeeehh

Ehhhh me najuta kubalehe

Ehhhh sikumbuki hata tarehe

Eeee ujana maji ya moto,zinaniunguza hizi starehe

Bridge{rich mavoko}

Heri ningerudi utoto,ujana maji ya moto

Eeeeeeeeh eeeeeh eeeeeeeh eeeeeeeehhh

Me najuta kubalehe,me najuta kubalehe eeeeeeh,me najuta kubaleeeeeeeeeeeeeehhhhhhhhh

Ontro{stamina}

Moro in da house,in da house

Moro town in da house,stamina in da house

Moro town in da house,stamina in da house

Ahahaha I luv hip hop