Released on November 24, 2022

Thumbnail

[Verse 1]

Hivi nachezea rhumba ama bolingo nangai

Maana nina kiwembe kwenye vita ya masai

Wanitesa mchumba nimependa sishangai

Penzi kitovu uzembe mi nalia we furahi

Ila musiende nyumbani za wageni walete nyumbani kwangu

Chunga taratibu na chaga msije vunja kitanda changu

Nimekunulia na feni msisweti mke wangu

Kama majasho mkimwaga litumie taulo langu


[Pre Chorus]

Naaa Baya lako zuri kwangu yote nimekusamehe

Kosa la kwako lawama kwangu acha tu nijitetee

Furaha yako furaha yangu sipendi unyong'onyee

Ukimpenda rafiki yangu sema nikutongezee

Utamu wa pipi ni mate yangu

Wapika na mimi wanakula wenzangu

Ona nakosa siti kwenye gari langu

Kuleni embe acheni kokwa langu


[Chorus]

Nateswa nateswa

Mwenzenu nateswa na mapenzi

Jamani nateswa nateswa

Mwenzenu nateswa na mapenzi


[Verse 2]

Mapenzi anapanga maanani sitaki kuruka kuruka

Sawa ni pande kichwani ukichota itashuka

Niite mfanyakazi wa ndani huna haja kusumbuka

Kwani anakuja muda gani niwatandikie shuka

Siogopi kushare ila usisahau kinga

Japo kwangu fedheha kuku wa chando nashinda

Kweli wanionea nakubali we ndo bingwa

Nipo radhi kulea kama wakikupa mimba


[Pre Chorus]

Naaa Baya lako zuri kwangu yote nimekusamehe

Kosa la kwako lawama kwangu acha tu nijitetee

Furaha yako furaha yangu sipendi unyong'onyee

Ukimpenda rafiki yangu sema nikutongezee

Utamu wa pipi ni mate yangu

Wapika na mimi wanakula wenzangu

Ona nakosa siti kwenye gari langu

Kuleni embe acheni kokwa langu


[Chorus]

Nateswa nateswa

Mwenzenu nateswa na mapenzi

Jamani nateswa nateswa

Mwenzenu nateswa na mapenzi