Tathmini

By Prof. Jay

Thumbnail

[Verse 1 – Professor Jay]

Naahidi kuwa makini mpaka siku nafukiwa chini

Na Mungu aliye hai bado yu pamoja na mimi

Emcee shika vizuri karibu tawi linakatika

Na kwa wote mliopo juu na chini sauti itafika

Kazi na dawa ndani ya uswazi kazi ni kazi

Na nipo radhi kutoa tathmini ngazi kwa ngazi

Rap si lelemama kama wengi mnavyodhani

Fasihi iliyo hai kuitoa jamii gizani

Miaka ya 80 Hip Hop Bongo ilichipua

Na nadhani wale wakongwe wa rap hii mnaitambua

Hali ilikuwa mbaya miaka ya 89

Watu hawakutaka kuelewa rap kabisa

Miaka ya 90 Hip Hop Bongo imekubalika

Wenye nia nzuri na rap tunawajibika

Rap ni wito yataka utashi na ufahamu

Elimu ya mtaani kujituma pia nidhamu

Wasanii wenyewe wa Bongo tunaofanya tudharauliwe

Watu vibongo vidogo hawataki washauriwe

Wanaongea blah blah, vijino viwe

Na wanaovunja hata miko ya rap waheshimiwe!

Wengine watatumia kivuli cha rap kufanyia uhuni

Hii ni sawa na kupanda ngazi kuelekea mbinguni

Tathmini ya kweli yatia majaribuni

Na mnaovunja miko ya rap jihukumuni

[Hook – Professor Jay] x2

Hii ni tathmini kwa wote juu na chini

Yoh emcee zunguka nyuzi 360

Umeona nini? Mwana mpotevu rudi kundini

Fani ni uwanja mpana na jua lipo utosini


[Verse 2 – Jay Moe]

Yoh! Mawazo ya Jay Moe usiku mchana yalikuwa wima

Ingawa sikujua usiku ukiisha asubuhi itakuwa neema

Kwani baba mama miaka ile kipindi cha nyuma

Waliamini rap ni kuimba yale yasiokuwa mema

Haina noma wakwezi tulipomaliza kusoma

Mistari iliandikwa ujumbe ukashuka ukakubalika

Ndio ilikuwa bado wenye hisa kutolea macho

Walithamini Bolingo, ambacho kimewachosha Bongo

Wahisani waongo, walidhani tungеdorola

Mara ngoma ika-change na nyota ya rap ikang’ara

Wasambazaji habari ya kwamba Hip Hop uhuni

Wameingia mitini ‘Chemsha Bongo’ ilipoingia rеdioni

Kama wametawala ikafika walio bungeni

Watu wakazinduka, yaani wakashtuka wataongea nini

Watu na Bongo Flava kingine wanasema uzushi

Taarabu imeingia nuksi, Bolingo inafuka moshi

Sasa wahisani tapeli hutuboa wenye mistari

Kila mtu anakuja na uongo ili mradi tukubali

Na ma-producer wa sasa wanashtuka kwamba tunauza

Wanashtuka kwamba walicheza, Hip Hop ina fedha

Jay Moe mbakiaji sasa nahitaji umaskini u-bounce

Shori mzuri, gari, pamba, fedha kwenye bank account

Labda tatizo iwe kwa emcee asiye na elimu

Eti afanye nini? Mi nadhani bora akauze ndumu

[Hook – Professor Jay] x2

Hii ni tathmini kwa wote juu na chini

Yoh emcee zunguka nyuzi 360

Umeona nini? Mwana mpotevu rudi kundini

Fani ni uwanja mpana na jua lipo utosini


[Verse 3 – Professor Jay]

Yule yule ni Jay na Jay ni yule yule

Wanga wekeni kikao kisha mnifanye msukule

Domo langu ni hela linatoa ushauri wa bure

Ila ma-emcee wengi wa Bongo hampendi kwenda shule

Kumbuka hii ni rap ndani ya karne ya 21

Ni lazma uchemshe bongo kwenye mchanganuo wa hoja

Nafurahi kuona emcees ni wengi kama utitiri

Kinachoniudhi wengi wana-rap bila kutumia akili

Rap ya Bongo imegawanyika makundi mawili

Na kuna ma-emcee kamili na emcee waliobatili

Emcee mwenye hekima anafikiri kabla ya ku-rap

Na emcee mpumbavu ana-rap apate nyapu

Natumia lugha kali tafsiri unavyoweza

Napunguza tafsida maneno yanajieleza

Watu viwango vidogo wanaleweshwa na sifa

Ni lazma mjikongoje kwenye level za kimataifa

Wengi hampendi kuchambua temethali za semi

Na matokeo ndo vile ngoma zenu mwali hanemi

Watu wanavaba mic na ku-rap kama majuha tu

Katikati ya bahari mnapanda boti za mabua

Msilete utani, hii ni fani yenye ushindani

Jiulize waliovuma wangapi wamebaki gizani

Ninaowaudhi, hii naifanya makusudi

Ili mpate ghadhabu na kuongeza juhudi

[Hook – Professor Jay] x2

Hii ni tathmini kwa wote juu na chini

Yoh emcee zunguka nyuzi 360

Umeona nini? Mwana mpotevu rudi kundini

Fani ni uwanja mpana na jua lipo utosini