Tabasamu

By Mr. BlueTZ

7K Views

Thumbnail

[Intro – Steve RnB]

Hey Hey Heyyyy

Heyyyy Mhhhh


[Chorus – Steve RnB]

Tabasamu nipate furaha

Usiwe unanuna baby, usiwe unauchuna wewe

Tabasamu nipate furaha

Usiwe unanuna baby, usiwe unauchuna wewe


[Verse 1 – Mr Blue]

Game kushuka na kupanda

Jana tumeshuka, cheki leo tumepanda

Tumepata idea ya kusambaza kanda

Nimepata shows za Kenya na Uganda

Burundi na Rwanda

Twende pamoja twende tukasake chanda

Mungu akijalia wanazuia kibanda, namiliki kiwanda

Tuko pamoja si ungefunga mkanda

Yote kwa sababu, nipe tabasamu

Tumechoka mitabu hii ndo time ya vitamu

Unapendaga club, unamkumbusha Lam

After two weeks turudi Dar Es Salaam

Tumetesa sana baby (sana, sana)

Vibaya ukinikana baby (uh uh)

Kuniona sina maana baby (uh uh uh uh uhhh)

Baby, toka mchana alfajiri

Chini utajiri, fake mpaka real

Mapen zi sio siri

Au kwa kuwa tuko wawili, mapenzi ndo ukaona siri?

Kama mabaya yanasemwa kila siku, daily

Wazushi nao hawaishi bifu

Maisha sio kutеsa kila siku

Japo pesa ndo kila kitu


[Chorus – Steve RnB]

Tabasamu nipate furaha

Usiwe unanuna baby, usiwе unauchuna wewe

Tabasamu nipate furaha

Usiwe unanuna baby, usiwe unauchuna wewe


[Bridge – Steve RnB]

Cheka kidogo ni wewe baby

Nione tabasamu lako girl

Mi naridhika, nafarijika

Ukinuna utaniumiza roho

Cheka kidogo ni wewe baby, oh

Mi naridhika, nafarijika, yeah

Tabasamu, tabasamu

Baby, baby


[Verse 2 – Mr Blue]

I say weka amazing smile wacha mi nisebenze

Achana na hao wanaosubiri niteleze

Boogie nami superstar tingisha hizo wezere

(Wezere) wezere, (wezere) wezere

Wakibana Bongo twenzetu kwa Madebe

Twende club zao twende tukaruke debe

Sikia hisia zao sio hisia ka za Reggae

Nawapiga bao wakijirudi kama Chege

Achana na wanga, wanga zao ni kutaga

Mitaa ya Upanga kule wanauza burger

Wanacheza Charanga, unacheza Ragga

Hisia za kimanga, sina hisia za kichaga

Basi baby si ungecheka kidogo

Hujui smile lako linaua mpaka vigogo

Halafu huko nature wala hutumii mkorogo

Pande za Masaki mpaka pande za Kigogo

Wamekutaka hawajakupata hata kidogo

Wakina Roma K, Abuu na Shebi Chogo

Hawajakupata hata kidogo

Haja-haja-hauja…

Blue vipi, mbona sikusikii tena?

Sikusikii uki-flow, mbona sikusikii usema?

Niko busy na baby jamani nishasema

Niko busy na wife jamani nishasema

Mabaya yanasemwa kila siku

Wazushi nao hamuishi bifu

Maisha sio kutesa kila siku

Japo pesa ndo kila kitu


[Chorus – Steve RnB]

Tabasamu nipate furaha

Usiwe unanuna baby, usiwe unauchuna wewe

Tabasamu nipate furaha

Usiwe unanuna baby, usiwe unauchuna wewe