Released on June 6, 2017

7K Views

Thumbnail

[Verse 1]

Hhhmmm

Nikutume wapi sasa njiwa

Uende unitafutie kipenda roho

Hhhmmm

Yuuh wapi kama unanisikia

Fanya unisaidie usichikoe ohhh

Tumia wako ujasiri na machachali

Chumvi sukari niwekeeeee

Nenda na ufike mbali

Ukipata hodari usisubiri nilete


[Bridge]

Ila sitaki kunguru mimi ehhh

Akaiba ndani

Kutwa kuzulula mitaaani kula mifupa

Asiyojua penzi nini (eeeh)

Wala shukurani (eeeh)

Chochote anakula hata kile kinachonuka


[Chorus]

Akanifanya nikawaaaa

Teja wa mapenzi

Nikawa mimi

Teja wa mapenzi

Akili ikasinizia ehh

Teja wa mapenzi

Ohhh masikini

Teja wa mapenzi

Moyoni ntaumia ehhh


[Verse 2]

Mama alisema penzi sherehe

Si mabomu ya machozi kutwa kulizana

Na ujana ukiendekeza starehe

Yule mwenye jema penzi utamuona hana maana

Mapenzi sio upinzani ule wa simba na yanga

Tuishi kama vitani kushikiana mapanga

Mapenzi kamari uyapati kwa waganga

Nishapiga sana tunguri nikaishia kutanga tanga

Ndo maaana


[Bridge]

Sitaki kunguru mimi ehhh

Akaiba ndani

Kutwa kuzulula mitaaani kula mifupa

Asiyojua penzi nini (eeeh)

Wala shukurani (eeeh)

Chochote anakula hata kile kinachonuka


[Chorus]

Akanifanya nikawa

Teja wa mapenzi

Nikiwa mimi

Teja wa mapenzi

Akili ikasinizia ehh

Teja wa mapenzi

Ohhh masikini

Teja wa mapenzi

Moyoni ntaumia ehhh


[Outro]

Na moyo akautia pancha

Pancha pancha ehhhh panchaa

Akautoboa

Pancha pancha ehhhh panchaa

Kila kona ukaweka viraka

Pancha pancha ehhhh panchaa

Eeeh onananalilaaaa

Pancha pancha ehhhh panchaa

Badala ya nazi nikapewa kidaka

Pancha (Ahhhhahah) pancha ehhhh panchaa

Ahhhhahah

Pancha pancha ehhhh panchaa

Wasafiiiiii