Kemosabe

By Fid Q

Released on August 13, 2015

11K Views

Thumbnail

Niliamini mapene hayatoshi..na niki-hustle siyakosi/

Sababu.. sipo kwenye loss na life simple huwa hai-cost/

Kwahivyo nikaenda Dar na treni... of thoughts../

Sikwenda kuzubaa au kushangaa nikusaka chapaa boss/

Sikutaka kuivaa mikosi..nilitaKa kuivaa mikoti/

Sikuwa na passport..password.. pin..lakini ni crack codes/

Walionisapoti wote siwaoni kwa line/

Wakini-approach ili nifungue pochi ya noti tu-shine..hatuko fine/

Je mimi ni kaka mubaya...? kaka aso haya../

KAKA..? huniitaga NAKAAYA/

Mama C huniita brother bila shaka.. Mozaya/

Niko sick & tired of being sick & tired/

Na huu ni mwaka wa ndui/ Sitaki upele urudi tena.. mnachotaka sikijui/

Nashukuru hamtopata mbawa ikiwa mtaupata huo uchui/

Mnautaka uadui? mnayempaka ni mtata.. makaka hamkui?

Mmeendekeza hila.. legeza hasira za harakati/

Mie nita-ball.... hata kwa mpira wa makaratasi/

Unaweza ukahisi mie napita tu.. kwakusahau mie nina-hustle/

Nimezaliwa Afrika.. ugumu wa maisha umenifunza ku-struggle/

Ukiwa idle.. unamu-attract shaytwan (SHETANI)/

Kichwani nina MSAHAFU na BIBLE.. life ni zaidi ya ku-have fun/

Kwani.. Kila kicheche anajiona ni mzima/

Na njia pekee ya kuepuka ngoma ni kugoma kupima/

Ikiwa maujuzi haya hayakugusi.. itanilazimu nikuelewe/

Sometimes hata kamusi.. huimiss tafsiri yenyewe/

Nalindwa na dua za mama.. tangu baba simjui/

Namfanya adui mwenye njama aache drama na akue/

Ili ajijue kabla hajakwama huko mrama asitue/

Ajikwamue kwenye lawama.. yenye maana yamchukue/

Kisha anaiombee mimi ili nifaidike kwa hizi mbio/

Siamini kwenye umasikini hivyo sihofii mafanikio/

Ndiyo.. mie ni LEO kwahiyo sifikirii kushindwa/

Zingatia kauli hiyo hausikii inaashiria ubingwa?/

Mie ni mbishi.. muulize Nikki - hatopinga/

Na hata kama ningekua mbuzi ningelala chaka la simba..